Ni Makala yanayoangazia kwa jicho la tatu mazingira halisi ya dunia yalivyo bila kusahau kile ambacho kinachangia kuyaharibu. Utapata kufahamu namna ambavyo mazingira na rasilimali zinavyoharibiwa huku pia teknolojia ikijumuishwa. Hakika mazingira mazuri ya leo ni dunia yako kesho.
Matumizi ya ufadhili wa hali ya hewa imekuwa swala kuu kwa wadau wa mazingira, kutokana na mianya ya ufuatiliaji. Nchini Kenya, shirika la Transparency International , sasa linajaribu kuziba mwanya uliopo ambapowakenya watakuwa wakifuatilia miradi na matumizi ya fedha hizi nchini humo kupitia jukwaa jipya la mtandaoni la Climate Finance Watch Tool.
Kwa wavuvi katika ziwa Niavasha, kama vile Simon Macharia na Joseph Kimani, Magugu maji yamekuwa kero kwa muda mrefu, na wakati mwingine kuwasababishia hasara. Lakini sasa kutokana na ubunifu wa Joseph Nguthiri , kijana bingwa wa dunia wa Mazingira wa UNEP mwaka wa 2025, na mwanzilishi wa kampuni ya Hyapak wavuvi wanaweza kujipatia kipato zaidi.
Familia katika kijiji cha Kihoto mjini Naivasha, zimeendelea kutaabika kutokana na athari za kupanda kwa kiwango cha maji kwenye ziwa Naivasha, na kusababisha maji kuingia kwenye kijiji ambayo pia yamesababisha kuenea kwa magugumaji. Nikurejesha nchini kenya, katika eneo la bonde la ufa, ziwa Bogoria, ziwa Baringo na Ziwa Niavasha, ni mfano wa maziwa ambayo yameendelea kushuhudia kupanda kwa kina…
Hali ya hewa ya El Niño inaendelea kuimarika kwa kasi na inatarajiwa kutawala katika kipindi cha kuanzia mwezi Agosti hadi Oktoba mwaka wa 2026, hali itakayoongeza uwezekano wa viwango vya joto kuzidi wastani katika maeneo mengi ya dunia na kusababisha mabadiliko makubwa katika mifumo ya mvua. Mashirika ya hali ya hewa likiwemo lile la dunia WMO na KMD nchini Kenya, yameongeza utaratibu, huduma za…
Wimbi la joto kali limekumba bara la Ulaya kwa muda sasa, hali iliyosababisha viwango vya juu vya joto katika nchi kadhaa na kusababisha maelfu ya vifo. Zaidi ya watu 300,000 wamehamishwa na angalau mtu mmoja alifariki dunia kutokana na moto wa nyika nchini Ufaransa na Uhispania, huku vikosi vya zimamoto vikipambana na mioto hiyo. Leo katika uchambuzi wetu tunaungana na Daktari Joyce Kimutai,…
Wakati mataifa mbalimbali duniani yakiongeza juhudi za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na uchafuzi wa bahari, nchini Kenya akina mama wamejitokeza mstari wa mbele kulinda mazingira. Katika Kaunti ya Mombasa, wameanzisha kampeni ya kupanda miti ya asili na kurejesha uoto uliopotea kwenye maeneo ya pwani. .Hii leo katika makala mazingira leo dunia yako kesho ,tunaangazia juhudi za…
Misitu ni sehemu muhimu katika mapambano ya dunia dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, hata hivyo misitu mingi ipo hatarini kutokan ana shughuli za binadamu. Fahamu kuhu mkaa unaotengenezwa kutokana na mmea wa mianzi(Bamboo)
Mkutano huo ulioandaliwa na Global Covenant of Mayors for Climate and Energy (GCoM kwa ushirikiano na UN-Habitat, ulijadili mada tofauti kama vile sayansi ya tabianchi, sera na namna ya kuangazia mianya iliopo katika elimu, data, ufadhili na utakelezaji zinazolemaza mikakati ya kukabili tabainchi kwenye miji. Katika makala yetu hivi leo, nimezungumza na Bi Maryam Wangeshi , ni msanifu wa majengo…
Kila wiki, mamilioni ya nguo za mitumba hufika katika masoko kama vile Gikomba jijini Nairobi, Kenya, au Kantamanto mjini Accra, Ghana. Takriban asilimia 40 ya bidhaa hizi zinazoagizwa kutoka nje haziwezi kuvaliwa kabisa, na hivyo kuhamishia mzigo wa udhibiti wa taka za nguo kwa jamii. Nguo nyingi zilitotengenezwa kwa kutumia poliesta na nailoni, huziba njia za maji za mijini, huchafua fuo za…
Tunawaangazia wadau muhimu katika sekta ya usimamizi wa takan hapa tunazungumzia wakusanyaji taka, ambao mara nyingi mchango wao hupuuzwa nasa katika meza ya maamuzi kuhusu suala hili la cuhafuzi wa taka.
Tatizo la uchafuzi wa mazingira kutokana na taka ngumu, bado ni changamoto katika miji mingi barani Afrika. Hata hivyo, hivi karibuni, kumekuwa na jitihada kwenye baadhi ya mataifa ambapo sasa nchi zimeanza kuwa na sheria na kanuni za kuhakkisha usimamizi endelevu wa taka, kwa kuwahusisha wazalishaji na waagizaji wa bidhaa.
Kwa muda mrefu maeneo ya nyanda za malisho yamekuwa yakitazamwa kama yaliotengwa na yasio na umuhimu, licha ya kuwa na mifumoikolojia muhimu na chanzo cha riziki kwa takriban watu bilioni mbili duniani, Pamoja na kuhifadhi theluthi moja ya hewa ya kaboni duniani. Lakini sasa wadau wa mazingira, watunga sera, watafiti, wataalam na wawakilishi kutoka jamii za wafugaji baranai Afrika sasa wanatoa…
Nairobi ni mwenyeji wa msitu mkubwa wa mvua ulio salama ndani ya mipaka yake: Hifadhi ya Karura yenye ukubwa wa hekari 1,000 ni mapafu muhimu ya mji mkuu wa Kenya, katika kuchuja uchafuzi wa mazingira kwa mamilioni. Ilikuwa ishara ya ukosefu wa usalama, sasa ni mfano mkuu wa kimataifa wa uhifadhi unaoongozwa na jamii haswa shirika la marafiki wa Karura maarufu Friends of Karura. Hata hivyo, msitu…
Msikilizaji, juma moja lililopita, mawaziri kutoka karibu mataifa 50 duniani walikutana nchini Colombia kwa mkutano wa mazingira uliolenga kujadili mbinu za mataifa kuachana kikamilifu na nishati zinachafua mazingira ikiwemo gesi na mafuta. Mjadala kuhusu mataifa kuachana na matumizi ya nishati chafu zinazochangia ongezeko la joto duniani, umekuwepo katika mikutano tofauti ya kimataifa ya…
Nchini Kenya, mzozo wa rasilimali katika jamii zinazopatikana katika maeneo kame ni changamoto ya muda mrefu, na kumekuwa na jitihada ya mashirika tofauti kuziwezesha jamii hizo kustahimili changamoto zitokanazo na athari za mabadiliko ya tabianchi. Kupitia mradi wa IMARA, jamii ya wafugaji sasa wamegeukia ukulima wa aina tofauti ambao baadhi yao unawadsaidia hata kupata chakula ya mifugo wao.
Mkutano wa pili wa Umoja wa Afrika unaofahamika kama 'Jukwaa la Mijini Afrika (AUF) ulianzishwa kwa nia ya kuwezesha mazungumzo na uratibu wa ukuaji endelevu wa miji na makazi ya watu barani Afrika. Pamoja na Maryam Wangeshi , msanifu wa majengo, tunaangazia matokeo ya mkutano huo na ikiwa mataifa ya Afrika yana mipangilio ilio bora katika kuwezesha miji yetu kustahimili majanga ya kimazingira.
Mimea ya mianzi yaani Bamboo ni mojawapo ya mimea kote ulimwenguni inayoweza kupandwa katika mazingira tofauti kama vile sehemu tambarare au chemichemi. Ukulima wa mianzi unaboresha mazingira kwa kuzuia mmomonyoko wa udongo, kurejesha rotuba kwa udongo haswaa sehemu zilizo karibu na mito na hata kama kitega uchumi.
Katika awamu ya kwanza tuliangazia uluhimu wa maeneo ya ardhi poevu katika mazingira, ikiwa ni pamoja na kutumika kama makazi ya aina tofauti ya spishi ya viumbe hai lakini pia ni mazalia ya samaki. Sasa ardhioevu ya Ondiri ni nyumbani kwa zaidi ya spishi 90 za ndege, Kwa mfano, tulifanikiwa kumuona ndege aina ya Korongo ambao mara nyingi wao hutoroka katika ardhioevu ambayo mazingira yake…
Vijana katika shirika la uhifadhi la Marafiki wa ardhi oevu ya Ondiri, ambayo ni nyumbani kwa viumbe hai na bayoanuai yenye umuhimu katika mazingira. Katika mazingira, maeneo haya yanya faida kama vile, kufanya kazi kama sponji ya kunyonya hewa ukaa kutoka kwenye anga zaidi ya misitu ya mvua. Hutumika kama makazi ya aina tofauti ya spishi ya viumbe hai lakini pia ni mazalia ya samaki. Ardhi oevu…
Wakulima wa Meru kaskazini mashariki mwa Kenya wanakumbatia matumizi ya mitego ya wadudu inayotumia nishati ya jua ili kukabiliana na false codling moth (FCM), mdudu anayeharibu mazao ya parachichi. Eneo la kaskazi mashariki huzalisha kiwango kikubwa cha parachichi zinazouzwa ulaya na Asia Kupitia teknolojia hii, wakulima sasa wameanza kupata nafasi katika masoko ya nje....vile vile wamepunguza…
Dunia inapokabiliwa na mgogoro wa mabadiliko ya tabianchi na changamoto zingine za kimazingira, je redio imekuwa na mchango gani katika kuhakikisha jamii zinapata taarifa na habari wanazohitaji kufanya maamuzi muhimu kuhusu mazingira yao.
Aliporejea madarakani Januari 20 2025, kwa mara ya pili Trump aliiondoa Marekani katika mkataba wa tabianchi wa Paris wa 2015. Mwaka wa 2025, Washington haikuwatuma maafisa wake wa juu katika mkutano wa tabianchi wa COP30, uliofanyika Belem, Brazil. Na sasa wiki chache zilizopita, utawala wa Trump ulitangaza kuiondoa Marekani katika mashirika 66 ya kimataifa, ikiwemo ile ya UNFCCC.
Upatikanaji wa nishati safi ya kupikia katika jamii kwenye vitongoji duni. Tumetembelea mtaa wa Kawangware, jijini Nairobi, kufahamu juhudi ambazo shirika la Umande Trust linafanya katika suala zima la upatikanaji wa nishati safi kwa kuzingatia usafi wa mazingira.
Upatikanaji wa nishati safi ya kupikia katika jamii kwenye vitongoji duni. Tumetembelea mtaa wa Kawangware, jijini Nairobi, kufahamu juhudi ambazo shirika la Umande Trust linafanya katika suala zima la upatikanaji wa nishati safi kwa kuzingatia usafi wa mazingira.
Katika maeneo mengi ya kusini mashariki mwa Kenya, ukame na mvua zisizotabirika zimekuwa changamoto kubwa kwa wakulima. Hata hivyo, katika kijiji cha Gachuriri, Mbeere, teknolojia rahisi ya umwagiliaji mimea maji kwa kutumia sola tembezi inayotumia nishati ya jua inaanza kubadili kilimo na kurejesha matumaini kwa wakulima wadogo.