Jua Haki Zako ni makala yanayokuelimisha juu ya umuhimu wa kufahamu haki zako na sheria halali zilizomo kwenye jamii, mataifa na dunia kwa ujumla. Jua Haki Zako itakuelimisha juu ya masuala mbalimbali ya kisheria ndani ya Afrika Mashariki, Afrika na Duniani kwa ujumla.
Utafiti wa punde zaidi uliofanywa na Kituo cha Utafiti wa Idadi ya Watu na Afya barani Afrika (APHRC) unaonyesha kuwa, Kusini mwa Jangwa la Sahara, msichana mmoja kati ya wanne anapata ujauzito kabla ya kufikisha miaka 18. Ingawa sheria na sera katika nchi mbalimbali katika ukanda wa Afrika Mashariki zinatambua haki ya wasichana hao kuendelea na masomo hata baada ya kujifungua, wengi bado…
Nchini Kenya changamoto za kupata stakabadhi muhimu kama vile vitambulisho na vyeti vya kuzaliwa zingali zinashuhudiwa miongoni wa raia wake hususan kwenye jamii ambazo zinaishi kaunti za miapakani kama vile Busia ,Turkana na Mandera, hali inayoendelea kuwanyika raia hao haki zao za kimsingi na kukosa huduma muhimu za serikali . Hii leo katika makala Jua haki zako tunaangazia akina mama hao na…
Nchini Kenya, mawakili wameandamana kudai haki kufuatia vifo vya wenzao wawili ambao wameuawa katika mazingira tata. Kwenye makala haya tunaangazia malalamishi ya mawakili hao. Sikiliza makala kufahamu mengi.
Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu Amnesty International, limeangazia namna gani wapiganaji wa rsf walikiuka sheria wakati wakiteka mji wa El Fasher. Skiza makala haya kufamu mengi
Awamu ya pili makala haya yanaendelea kuangazia haki za wakimbizi mawakili Maasai Mutune na Rajab Membe, kutoka shirika la Refugee Led Organization Network nchini Kenya, wanajadili haki hizo. Skiza kufahamu mengi.
Kila Juni 20 dunia huadhimisha siku ya wakimbizi duniani, juma hili mawakili Maasai Mutune na Rajab Membe, kutoka shirika la Refugee Led Organization Network nchini Kenya, wanajadili haki za wakimbizi. Skiza makala haya kufahamu mengi.
Lydia Mwende mwanamitindo na mwanaharakati ni mchanga ambaye amejitokeza kupinga mimba wa utotoni nchini na pia kulelewa na mzazi mmoja. Sikiliza makala haya kufahamu msimamo wa Mwende.
Wanawake wanaotetea haki za kijinsia katika eneo la Pwani nchini Kenya wameonya kuhusu ongezeko la visa vya ukatili wa kijinsia, wakisema ukosefu wa elimu kuhusu haki za waathiriwa unawazuia wengi kupata haki. wanaharakati hao wanasema hali hiyo imechangia wahusika wa vitendo vya ubakaji, ulawiti na unyanyasaji wa kingono kuendelea kutenda makosa bila kuwajibishwa. Skiza makala haya kufahamu…
Katika makala ya Jua Haki zako, tiunazumgumza na waathiriwa waili wa ukatili wajinsia katika mtaa wa Mathare, Benedicta Musalizi na Cathrene Maina pamoja na mwanaharakati ambaye anapigania hazi za waathiriwahawa katika mtaa wa Mathare Bi. Beatrice Karore.
Mzalishaji wa muziki nchini Kenya Motive Di Don kwa ushirikiano na benko moja nchini humo wameanzisha ushirikiano wa kuwasaidia wanamziki chipkizi ndani ya mradi wa Eleve8. Skiza makala haya kufahamu mengi.
Kila mwezi Mei dunia huadimsha siku ya uhuru wa nyombo vya habari na wanahabari. Katika makala haya tunaangazia changamoto wanazopitia wanahabari wakati wakitekeleza majukumu yao.
Licha ya kuongezeka kwa idadi ya wanawake wanaojihusisha na biashara za kimataifa nchini Kenya, wengi wao bado wanakumbana na changamoto kubwa,ikiwemo kudhalilishwa, ubaguzi wa kijinsia na kunyimwa haki zao za msingi wanapojaribu kuingia au kushindana katika masoko ya nje. Katika maeneo ya mashambani hadi mipakani, wanawake hawa wanapambana si tu kukuza biashara zao, bali pia kupigania heshima na…
Katika makala haya tunajikita kuangazia mchango wa mashariki yasiokuwa ya kiserikali kwenye jamii zetu. Tunaliangazia shirika la Corps Africa ambalo kwa ushirikiano jamii mbali mbali nchini Kenya limeendelea kuleta mageuzi kwa raia. Ili jamii kuendelea na kujitegemea inahitaji watu wa kufanikisha baadhi ya maswala kwa jamii kuja na mbinu ya namna gani ya kuwezesha jamii kujiendeleza. Kutokana na…
Katika makala haya tunaangazia ripoti kuhusu ufadhili wa majanga na mabadiliko ya tabianchi katika maeneo kame, iliochapishwa na masharika kadhaa likiwemo lile la Oxfarm. shaba ikilenga taifa la Kenya, Ripoti hii inaonyesha kuwa licha ya maeneo haya kuathirika zaidi na ukame, mafuriko na mabadiliko ya tabianchi, bado fedha nyingi hazifiki moja kwa moja kwa wananchi wanaohitaji msaada huo zaidi.…
Katika makala haya tunaangazia haki za wafanyibiashara katika soko la Gikomba nchini Kenya. Kwa muda wafanyibiashara hao wamekuwa wakizozana na serikali kuhusu kipande cha ardhi cha soko hiyo. Skiza makala haya kufamu mengi zaidi.
Kila mtotto ana haki kwa mjibu wa katiba za kila nchi na maazio ya kimataifa. Katika makala haya tunaanhazia haki za watoto wa kurandaranda mitaani. Skiza makala haya kufahamu mengi.
Kila Machi nane dunia, huadimisha siku ya kimataifa ya wanawake, katika makala haya tunaangazia sababu ambazo zimechangia wanawake kuachwa nyuma katika harakati za kutafuta amani. Skiza makala haya kufahamu mengi.
Nchini Kenya tume ya kupambana na rushwa EACC imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha mali ya umma haiporwi. Ila ni mchakato upi mtu anastahili kufuata kutoa taarifa kwa tume. Benson Wakoli alikiti chini Kipsang Sambae afisa wa EACC, tawi la Nakuru kufahamu mchakato wa kutoa taarifa kwa EACC.
Makala haya yanaangazia ripoti ya Human Rights Watch iliyochapishwa tarehe 4 Februari 2026, inayozungumzia hali ya kutisha ya haki za binadamu katika eneo la Pembe ya Africa. Ripoti hiyo inaonyesha kuwa raia wa Sudan , Sudan Kusini na Ethiopia ndio wanaobeba mzigo mkubwa wa vita vya silaha vinavyoendeshwa kwa ukatili, ambapo pande zinazopigana mara nyingi hulenga raia kimakusudi. Human Rights…
Kwa miaka mingi Beatrice Karole amekuwa akijitolea kuhamasisha jamii kuhusiana na hatua za kuchukua wakati wanapokabiliana na unyanyasaji wa jinsia. Akiwa na shirika la kinamama la Wanawake Mashinani Initiative katika eneo la Mathare Jijini Nairobi, amefanikiwa kuwaokoa jumla ya wanawake na watoto 30 katika mwaka 2025 ambao anajivunia kuwa licha ya kunyanyaswa, walipata haki yao.